Powered By Blogger

Ijumaa, Mei 26, 2017

RAMADHANI KAREEM : Waislamu waanza kufunga kesho

Waumini wa dini ya kiislamu kote ulimwenguni wanatarajiwa kuanza kutekeleza ibada ya swaum kuanzia kesho ama kesho kutwa kulingana na kuandama kwa mwezi.
Saum ni nguzo ya nne ya dini ya kiislamu ambapo hujizuia na kula na kunywa hadi jioni pamoja na kutekeleza ibada kwa wingi.
Viongozi wa dini ya kiislamu katika kaunti ya Taita Taveta sasa wanaitaka serikali ya kitaifa kuhakikisha kuna usalama wa kutosha katika maeneo ya ibada na hasa misikiti wakati huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhan unapoanza.
Also read:

Mahakama yahahirisha kesi ya kuwaadhibu madaktari wanaogoma

Wakiongozwa na mwenyekiti wa baraza kuu la waislamu katika kaunti ya Taita Taveta Washallah Abdhi,wanasema mwezi huu ni muhimu kwa kalenda ya jamii ya waislamu na ni sharti usalama uimarishwe kuwezesha jamii hio kutekeleza ibada zao bila matatizo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni