Powered By Blogger

Jumatano, Mei 10, 2017

Rais Jackob Zuma atua nchini ikiwa ni ziara yake ya 3

Dar es Salaam. Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma amewasili nchini leo (Jumatano) usiku.

Rais Zuma atakuwa nchini kwa ziara ya siku tatu kufuatia mwaliko kutoka kwa Rais John Magufuli.

Ziara ya Rais huyo hapa nchini inalenga kuimarisha uhusiano wa kibiashara kati ya Tanzania na Afrika Kusini.

Katika ziara hiyo Rais Zuma anatarajiwa kushiriki mkutano wa wafanyabiashara, kuzindua jengo la Ubalozi wa Afrika Kusini na kutembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni