Powered By Blogger

Jumatatu, Mei 08, 2017

Askofu afunguliwa mashtaka baada ya kuoa Mke wa Mu umini wake

Karagwe. Mchungaji wa kanisa la huduma katika roho wilayani Karagwe, Jafece Josephat anashikiliwa na jeshi la polisi wilayani humo baada ya kumuoa mke wa muumini wake na kuanza kuishi naye kama mke na mume akidai ameoteshwa na Mungu.
Mchungaji huyo amekamatwa leo baada ya kamati ya ulinzi na usalama na kamati ya amani na maadili ikiongozwa na mkuu wa wilaya hiyo, Godfrey Mheruka kufika kanisani hapo na kupata ukweli juu ya jambo hilo baada ya pande zote akiwemo mchungaji wa kanisa Josephat, mwanamke aliyefahamika kwa jina la Domina Damian na mme wake wa mwanzo Donath Appolo kueleza ukweli jinsi walivyooteshwa mpaka hatua ya mke kuolewa.
Mheruka alitoa agizo la kukamatwa kwa mchungaji huyo kutokana na baba wa Appolo aliyenyanganywa mke kujitokeza mbele ya kanisa hilo na kudai mahari aliyomtolea mtoto wake irudishwe kwani hawezi kuutolea mahari ukoo mwingine kwa kuwa mke ameshaolewa na mme mwingine.
"Kwa kuwa, mke ameacha familia yake akaja kuolewa na wewe mchungaji amezini na kwa kuwa wewe unayejiita mchungaji umeiacha familia yako ya watoto watano ukaoa mke mwingine nyote mnazini kwani kinachotenganisha ndoa ya mke na mme ni kifo lakini nyie mmejichukulia maamuzi yenu binafsi,"amesema Mheruka.
Mheruka amemwagiza mwangalizi wa kanisa hilo kuendelea kutoa huduma katika kanisa hilo ndani ya miezi sita huku akitafuta utaratibu wa mchungaji mwingine mwenye maadili mema na kuwa wao kama Serikali watachunguza vizuri kama kanisa hilo limesajiliwa au halijasajiliwa ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa.

Nitumie maoni yako Kupitia Facebook.com/proffesa%nazirhamzatz

RAIS JOHN POMBE MAGUFULI ASIKITIKA SANA KUTOKANA NA AJALI ILIYOTOKEA KARATU_MKOANI ARUSHA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ametoa neno na kusema amepatwa na uchungu na majonzi baada ya kuona majeneza ya watoto na walezi wao ambao walipata ajali ya basi huko Arusha.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.


Rais Magufuli amesema hayo kupitia ukurasa wake wa twitter na kuwataka Watanzania kuomboleza msiba huu kwa umoja huku tukiwaombea marehemu hao wapumzike mahali pema peponi.

"Nimepatwa na uchungu na majonzi makubwa ninapoyaona majeneza ya watoto na walezi wao waliopoteza maisha katika ajali ya basi huko Arusha, tumewapoteza mashujaa wetu katika elimu. Tuwaombee na tuendelee kuwa na subira, uvumilivu na ustahimilivu, tunapoomboleza vifo vya wapendwa wetu tuendelee kuwa wamoja. Mungu ibariki Tanzania" alisema Rais Magufuli 

Mbali na hilo miili yote ya marehemu ambayo imeagwa leo katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha imesafirishwa na kuelekea sehemu mbalimbali za nchi kwa ajili ya ndugu kufanya maziko ya wapendwa wao hao.  

MOMOGORO BLOG : Salaamu za lambi lambi kutoka wizara ya afya na mpango wa jamii zatolewa

Nazir Hamza : Salaamu za lambi lambi kutoka wizara ya afya na mpango wa jamii zatolewa

MOMOGORO BLOG : Salaamu za lambi lambi kutoka wizara ya afya na mpango wa jamii zatolewa

Salaamu za lambi lambi kutoka wizara ya afya na mpango wa jamii zatolewa

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepokea kwa huzuni na masikitiko  makubwa taarifa ya vifo vya watoto 32, walimu 2 na dereva mmoja wa shule ya Lucky Vicent ya Arusha, vilivyosababishwa na ajali ya gari iliyotokea katika eneo la Rhotia Marera, Wilaya ya Karatu - Arusha. 

Tunasikitika sana kwa kuwa ajali hii imetokea wakati wazazi, walezi na walimu wakitekeleza wajibu wao wa msingi wa kumpatia mtoto haki ya kuendelezwa Kielimu.

Kufuatia msiba huu mkubwa, kwa niaba ya Wizara na kwa niaba yangu mwenyewe ninatoa pole kwa wazazi, walezi, familia na jamii yote ya Arusha na Tanzania kwa ujumla, kwa kupoteza watoto wetu ambao walikuwa wanaandaliwa kuwa nguvu kazi ya Taifa letu katika Sekta mbalimbali. Tunamuomba .

 

Mwenyezi Mungu awapatie Faraja na Moyo wa Subira  katika kipindi hiki kigumu cha huzuni, uchungu na simanzi kwa familia za marehemu na Taifa kwa ujumla. 

Tunaziombea roho za watoto wetu wapendwa zipumzishwe mahali pema peponi, Amiin. Ni maombi yetu pia kuwa Majeruhi waliopo hospitalini watapata nafuu ili waweze kuendelea na masomo.

Ummy Mwalimu, Mb

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

07/05/2017

Nazir Hamza : Ajali mbaya iliyotokea Arusha Jana Asubuhi , baadhi ya wanafunzi wakiingizwa hospitalini


Nazir Hamza : Ajali mbaya iliyotokea Arusha Jana Asubuhi , baadhi ya wanafunzi wakiingizwa hospitalini