Jumamosi, Januari 20, 2018
Hizi ndizo sehemu kuu 10 zenye msisimko mkali kwenye mwili Wa mwanamke
Mazoea ya kufanya mambo yaleyale kila siku kwa muda mrefu hufanya tendo hilo la ndoa lianze kua baya na huenda ikawa chanzo cha mtu kuchepuka kutafuta ladha zingine.
Kitaalamu katika sayansi ya binadamu kuna maeneo kadhaa ambayo wanawake wote wakiguswa hupata msisimko mkali lakini msisimko hutafautiana kutokana na mwanamke husika kama ifuatavyo.
1. Kichwani; juu ya kichwa cha binadamu kuna mishipa mingi ya damu na ile ya fahamu hivyo maeneo haya yakishikwa homoni kama oxytocin na serotoinin huachiwa mwilini na kuleta msisimko mkubwa.
Jinsi ya kufanya; mshike kwanzia nyuma ya sikio kisha ingiza vidole katikati ya nywele kama unamkuna kichwa bila kutumia nguvu.
2. Sikio; sikio ni sehemu yenye mishipa ya fahamu inayoenda kwenye ubongo, mara nyingi sikio watu hua wanalipuuza sana na kuzani halihusiki lakini naomba nikwambie ni moja ya sehemu inayoweza kumfanya mtu achanganyikiwe.
Jinsi ya kufanya; anza kwa kumnong'oneza kwa sauti nzito, kisha libusu sikio lake baada ya hapo unaweza kulamba sehemu ya sikio la nje na baadae kuingiza ulimi ndani ya sikio kabisa. hapa msisimko ni mkali sana na anaweza kukukwepa na kutoa sauti kali ya kimahaba.
3. Ulimi ; ulimi ni sehemu ya mwili ambayo ina mishipa mingi mara mia moja zaidi kuliko ile mishipa ya fahamu ya viganja vyetu. msisimko wa ulimi unasababishwa kumwagika kwa homoni ambazo zinatuletea furaha ya mioyo yetu.
Jinsi ya kufanya; busu tu inatosha kusisimua ulimi wa mtu wako, bahati mbaya kuna watu hawajui kubusu. ukiwa unabusu mtu usipanue mdomo mzima kama samaki mfu... fungua mdomo wako kidogo kisha nyonya lips za juu wakati mtu wako ananyonya za chini na hii ndio busu linavotakiwa kua.
4. Shingo; hii ni sehemu ya mwili yenye ngozi laini sana ambayo inasisimka hata kwa kuipumulia tu na pua. ni moja ya sehemu nzuri sana kunyonya, kulamba na kubusu.
Jinsi ya kufanya; ukiwa umemkumbatia mtu wako basi busu upande wa kulia au wa kushoto wa shingo huku ukinyonya ngozi la eneo hilo.
5. Chuchu; wanaume wengi wanatumia sehemu hii kama sehemu kuu kumsisimua mwanamke, ni kweli kabisa tafiti zinaonyesha kwamba sehemu ya ubongo ambayo husisimuka chuchu za mwanamke zikiguswa ni sehemu hiyohiyo ambayo inasisimka kinembe na uke vikiguswa. kwa hiyo ni moja ya sehemu muhimu sana.
Jinsi ya kufanya; tomasa matiti yote ya mwanamke kwa kutumia mikono yako miwili kisha nyonya chuchu yake taratibu huku kama unaing'ata na kuiachia. badilisaha kwa kuchocha chuchu ya kulia na kushoto.
6. Kiuno au mgongo wa chini; kama umechunguza ni kwamba wanawake wengi husisimka sana wakiguswa viuno vyao ghafla hata wakati wa kukumbatiwa tu. hii ni sababu ya mishipa ya fahamu inayoenda hadi kwenye sehemu zake nyeti hupita huko.
Jinsi ya kufanya; tomasa kama unafanya masaji sehemu ya chini kabisa ya kiuno kabla makalio hayajaanza. hii itamfanya arelax sana lakini pia kuongeza damu kwenda sehemu zake nyeti tayari kwa tendo la ndoa.
7. Tumbo; tumbo ni sehemu ambayo watu wengi hawaitilii manani sana lakini misuli ya tumbo imeungana na uke moja kwa moja ndio maana baadhi ya wanawake hufika kileleni kwa kufanya mazoezi ya tumbo kitaalamu kama core exercises..
Jinsi ya kufanya; tomasa tumbo lake kwanzia juu kabisa ya tumbo na kwenda tumbo la chini na kisha busu taratibu maeneo mbalimbali ya sehemu ya tumbo na unaweza kumalizia kwa kunyonya kitovu.
8. Katikati ya mapaja; hii ni sehemu yenye msisimuko mkubwa kwenye mwili wa mwanamke, watu wanaondesha magari wanajua siri hii kwani wakimpakia mwanamke wanatumia njia hii kumsisimua kwa kuweka mkono mmoja kwenye mapaja yake.
Jinsi ya kufanya; shikashika sehemu za katikati ya mapaja kwanzia magotini kwenda mpaka karibu na uke.unaweza fanya hivyo wakati ukiwa unambusu.
9. Nyayo za miguu; nyayo za miguu zikiguswa hata kwa mtu ambaye sio wa kike zina msisimko sana kama wa kutekenywa hivi na sina msisimko mkubwa kuliko sehemu nyingi nilizotaja.
Jinsi ya kufanya; shika nyayo moja ya mguu kisha kwa kutumia viganja viwili tomasa katikati ya mguu kwanzia kwenye kisigino mpaka kwenye vidole.usitumie nguvu nyingi...
10. Kinembe [critoris]; hii ni sehemu ya mwanamke ambayo kazi yake ni kuleta msisimko tu na raha kwa mwanamke..eneo hili linazaidi ya mishipa ya fahamu 8000, ni eneo dogo sana lakini shughuli yake sio ndogo. naweza kusema ndio eneo lenye msisimko mkali kuliko yote niliyotaja hapo juu na likiguswa tu mwanamke analoana kabisa.
Jinsi ya kufanya; kidole chako kikubwa cha kinganyani bonyeza na kuachia sehemu hiyo kama mtu anayekagua parachichi pia sugua kwenda chini, juu na pembeni kuangalia muhusika anapenda wapi zaidi pia kama una uhakika na usafi au afya ya muhusika unaweza lamba lwa kuzungusha ulimi sehemu hiyo.
Mwisho; sehemu zote nilizotaja hapo juu ni muhimu sana kwa ajili ya kumuandaa mwanamke japokua kila mwanamke anapata msisimko zaidi kutokana na yeye mwenyewe alivyo yaani mwingine shingo linaweza kua na msisimko wa kawaida likiguswa lakini mwingine ikawa msisimo mkali zaidi.
Powered by
Jinsi ya kumpagawisha mmeo na akupende zaid na zaidi
Na kila ukiwa haupo machoni kwake kwa hisiaunazomsababishia anajikuta anakuwaza na kukufikilia wewe sababu ya kile kilichomoyoni mwake ni Zaidi ya mapenzi, ni Zaidi ya upendo, ni Zaidi ya historia yakuwa pamoja, ila ni uhuru wa kukupenda wewe kwa jinsi atakavyo, uhuru wakuongea na wewe kwa kila hisia ya neno na matamshi, ni utashi wa kupenda nakuyafurahia mapenzi na kuyafanya awe na raha kuyaacha yamtawale moyo nakukufanya wewe umtawale moyo wake kwa kila pigo linalompiga.
Kiumeni.com tunachokuambia sio sura yako au swaga zako ndo zitakazo mfanya msichana akupende Zaidi ya yeye atakavyo, ila ni kwa jinsi wewe unavyomfanya ajisikie akiwa nawe, jinsi anavyojihisi na kupokea upendo unaotoka moyoni kwake na kuukubali, ndicho kitu kikuu kitakacho mfanya mpenzi wako apagawe nawe na kujikuta akikupenda kupitiliza.
Yafanye mapenzi kwa mpenzi wako yawe zaidi ya hisia, zaidi yajinsi anavyojisikia akiwa na wewe, mfanye asipokuona aanze kukufikilia sio kwajinsi anavyokukosa pekee ila kwa jinsi anavyokosa zile hisia za furaha naupendo, hisia za uhuru wa kupenda, upendo uliomtamu maana unamfanya afurahiemapenzi, afurahie maisha kwa ujumla anayotumia na wewe, jinsi mnavyoongea,jinsi ulivyojenga ukaribu na yeye kiasi tofauti na mapenzi yalivyo, mna urafikitayari ulioshiba na kuelewana.
Hakikisha kila mda unaotumia nae unamtengenezea kumbukumbu nzuri, afurahie vitendo mnavyofanya pamoja na kutengeneza historia yenu wawili, kumbukumbu zinazomburudisha moyo wake kiasi hata ukiwa mbali na akazifikilia, zinamfanya atabasamu na hisia za kukumisi kumjaa mara dufu, hizo hisia za kumtaka awe tena karibu yako zimfanye asiache kukutafuta kwenye simu na kukutumia meseji.
Mfanye ajione tofauti, ajihisi unamwona spesho na sio kwa sifa unazompa ila kwa jinsi unavyomchukulia, aone kwa vitendo, aamini kwa macho yake mwenyewe, hii itamfanya akupende bila kujihisi, afanye vitu kwa jinsi mapenzi yanavyompeleka yeyewe, ajitoe kwa moyo na kukuona kuwa nawe ni bahati hivyo atajikuta anaitumia hio bahati kwa marefu na mapana, huku akiwa ajiulizi wala kujishuku.
“mara nyingi wanawake huwa na hofu ya kupenda, hofu ambayoinawatawala Sana na iwapo huwa unawasikiliza kwa makini utakuwa umeshaisikiahofu hii, sababu kuu ya hofu hii ni kuwa, wanawake wanaogopa kutendwa, wanahisiwakimpenda mwanaume kupitiliza, na huyo mwanaume akajua kutamfanya huyomwanamme kumshusha thamani mwanamke”,
Iwapo ukimwondolea hii hofu na kujikutaanakuamini kutamfanya akupende bila mipaka, bila mashaka na kukolea kwenyemapenzi Zaidi na Zaidi na Zaidi.
Powered by
©proffesa Momogoro
Je unataka kufanikiwa kimaisha mbinu hizi apa
Ijumaa, Mei 26, 2017
RAMADHANI KAREEM : Waislamu waanza kufunga kesho
Waumini wa dini ya kiislamu kote ulimwenguni wanatarajiwa kuanza kutekeleza ibada ya swaum kuanzia kesho ama kesho kutwa kulingana na kuandama kwa mwezi.
Saum ni nguzo ya nne ya dini ya kiislamu ambapo hujizuia na kula na kunywa hadi jioni pamoja na kutekeleza ibada kwa wingi.
Viongozi wa dini ya kiislamu katika kaunti ya Taita Taveta sasa wanaitaka serikali ya kitaifa kuhakikisha kuna usalama wa kutosha katika maeneo ya ibada na hasa misikiti wakati huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhan unapoanza.
Also read:
Mahakama yahahirisha kesi ya kuwaadhibu madaktari wanaogoma
Wakiongozwa na mwenyekiti wa baraza kuu la waislamu katika kaunti ya Taita Taveta Washallah Abdhi,wanasema mwezi huu ni muhimu kwa kalenda ya jamii ya waislamu na ni sharti usalama uimarishwe kuwezesha jamii hio kutekeleza ibada zao bila matatizo
Jumamosi, Mei 13, 2017
Kuhusu wenye vyeti feki kulipwa mafao
Watumishi waliobainika na vyeti feki, watalazimika kusubiri mafao yao hadi utaratibu wa kuwalipa utakapofanyika.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki alitoa kauli hiyo jana bungeni wakati akijibu swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Amina Mollel.
Amina alitaka kujua ni hatua gani zitachukuliwa ili kuwalipa mafao yao wafanyakazi waliobainika na vyeti feki.
Waziri Kairuki alisema, ofisi yake itaandaa utaratibu wa mafao ya wafanyakazi hao na pindi utakapokamilika, watajulishwa na kulipwa haki zao.
Aidha, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera , Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu, Anthony Mavunde, alisema kwamba seeikali inaendelea na mchakato wa kuunganisha mifuko ya jamii.
Mavunde alisema hayo alipojibu swali la msingi la Mbunge wa Tabora Kaskazini (CCM), Almas Maige, aliyetaka kujua mchakato wa kuunganisha mifuko ya hifadhi ya jamii, umefikia hatua gani.
Mavunde alisema, serikali kwa sasa inafanya tathmini ya mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo imetoa mapendekezo kuhusu namna bora na mambo ya kuzingatiwa katika mchakato wa kuunganisha mifuko hiyo.
Alisema, wadau vikiwemo vyama vya waajiri, vimeshirikishwa ili kutoa maoni na mapendekezo kwa serikali na kutoa maamuzi.
Proffesa J amshangaa Waziri mwakyembe kutaka wasanii wasiimbe siasa
Saturday, May 13, 2017 burudani, siasa

Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule maarufu kama Profesa Jay, ametoa maoni yake kuhusu ushauri wa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe aliyewataka wasanii wa Tanzania kuacha kuimba nyimbo zenye jumbe za kisiasa kwani hawatafanikiwa.
Profesa Jay ambaye ni rapa nguli wa kizazi kipya aliyewahi kuweka rekodi maalum ya albam yake ya ‘Mapinduzi Halisi’ iliyokuwa na jumbe zenye mlengo wa kisiasa na kijamii, amesema ameshangazwa na kauli ya Waziri.
“Kuwaambia wasanii kuwa waimbe nyimbo za maisha yao tu na washindwe kuimba vitu vingine, maana yake unataka kutoa ‘green light’ kwa wasanii sasa waanze kuimba mambo ya mapenzi… nakupenda, nakupenda..,” alisema Profesa Jay.
“Maana yake unaweza kuchochea kuhusu masuala ya mapenzi tu na kushindwa kufanya vitu vya kijamii ambavyo vingeweza kulipeleka taifa letu mbele. Mimi naamini msanii ana sauti kubwa na anaweza kupaza sauti positively na ikasaidia taifa letu ideologically (kiitikadi), socially (kijamii), culturally (kitamaduni), economically (kiuchumi), politically (kisiasa) pamoja na sustainable development (maendeleo endelevu),”aliongeza.
Mbunge huyo alidai kuwa wapo wasanii walioimba kuhusu siasa na masuala ya kijamii kama 2Pac, BIG, Bob Marley, Lucky Dube na wengine ambao walisaidia dunia kuhama katika ngazi moja kijamii hadi ngazi nyingine.
Hata hivyo, Profesa Jay alikubaliana na hoja ya Waziri Mwakyembe kuwa wasanii hawapaswi kuitukana Serikali, akieleza kuwa wanapaswa kuachwa watoe mawazo yao mbadala ikiwa ni pamoja na kuisifia Serikali.
Akizungumza Bungeni mjini Dodoma, Waziri Mwakyembe aliwashauri wasanii kuachana na nyimbo za siasa kwani hawatafanikiwa kwakuwa hakuna msanii ambaye alijikita katika kuimba siasa na akafanikiwa.
Kuhusu wenye vyeti feki kulipwa mafao
Watumishi waliobainika na vyeti feki, watalazimika kusubiri mafao yao hadi utaratibu wa kuwalipa utakapofanyika.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki alitoa kauli hiyo jana bungeni wakati akijibu swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Amina Mollel.
Amina alitaka kujua ni hatua gani zitachukuliwa ili kuwalipa mafao yao wafanyakazi waliobainika na vyeti feki.
Waziri Kairuki alisema, ofisi yake itaandaa utaratibu wa mafao ya wafanyakazi hao na pindi utakapokamilika, watajulishwa na kulipwa haki zao.
Aidha, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera , Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu, Anthony Mavunde, alisema kwamba seeikali inaendelea na mchakato wa kuunganisha mifuko ya jamii.
Mavunde alisema hayo alipojibu swali la msingi la Mbunge wa Tabora Kaskazini (CCM), Almas Maige, aliyetaka kujua mchakato wa kuunganisha mifuko ya hifadhi ya jamii, umefikia hatua gani.
Mavunde alisema, serikali kwa sasa inafanya tathmini ya mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo imetoa mapendekezo kuhusu namna bora na mambo ya kuzingatiwa katika mchakato wa kuunganisha mifuko hiyo.
Alisema, wadau vikiwemo vyama vya waajiri, vimeshirikishwa ili kutoa maoni na mapendekezo kwa serikali na kutoa maamuzi.
Wabunge wahuzunika sana kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha
Wakazi wa Videte Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani wakivuka mto Mzinga kwenda Bamia karibu na Uwanja wa Azam Complex Chamazi Manispaa ya Temeke Dar es Salaam. Wakazi hao wameomba kusaidiwa daraja kwa kuwa uvushaji huo ni hatari kwa maisha yao hasa kipindi hiki cha mvua. Wakazi hao wanavushwa kwa shilingi 1000 kwa kila kichwa.
ATHARI za mvua kubwa zinazoendelea kunyesha na kusababisha mafuriko na maporomoko katika sehemu mbalimbali nchini jana ziliwagusa wabunge na kutaka Bunge liahirishe shughuli zake ili wabunge waijadili hali hiyo iliyoathiri miumdobinu, makazi na hata kusababisha vifo.
Mvua hizo zinazoendelea kunyesha kwa takribani wiki tatu mfululizo sasa, zimeacha athari kubwa katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Dar es Salaam, Pwani, Tanga na Zanzibar. Wabunge walioomba mwongozo baada ya kumalizika Kipindi cha Maswali na Majibu ni Mbunge wa Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani (CCM), Mbunge wa Vunjo James Mbatia (NCCR Mageuzi) na wa Mlalo, Rashid Shangazi (CCM).
Ngonyani maarufu kama Profesa Majimarefu alisema kuna matatizo makubwa ya mafuriko nchini. “Kwenye mkoa wangu wa Tanga kumekuwa na maafa, leo (jana) hii kuna watu 1,000 hawana chakula, mahali pa kuishi na hawana msaada wowote, lakini serikali itawasaidiaje hawa watu wakati kamati za afya zikiendelea na utaratibu,”alisema. Kwa upande wa Shangazi alitaka shughuli za Bunge ziahirishwe ili wabunge wajadili kuhusu mafuriko hayo.
“Sasa hivi katika mkoa wa Tanga kuna mafuriko makubwa sana. Jana (juzi) yametokea maporomoko katika milima ya Usambara, eneo la barabara za Lushoto- Arusha- Mombo , Pangani kwenda Tanga, Mombo kwenda Lushoto na Kilindi kwenda Morogoro zote zilifungwa,”alisema.
Alisema Mkoa wa Tanga umegeuka kuwa kisiwa umepata athari kubwa hasa Korogwe na kuiomba Serikali ilione hilo jambo ni la kimkakati na kwamba Meneja wa Wakala wa Barabara (Tanroads) amezidiwa .
Alisema barabara hizo zimekuwa zikiunganisha mkoa huo na mikoa mingine na kutaka Bunge lijadili angalau kwa muda mfupi. Naye Mbatia alisema hali ni tete kutokana na mafuriko yaliyojitokeza na kuomba utu wa mwanadamu kuzingatiwa kama wawakilishi wa Watanzania kwa kutenga muda wa angalau dakika 15 kujadili suala hilo.
“Tutenge muda wa dakika 15 ama 20 ili tujadili suala hili, ambayo ni ya maafa tunaweza tukatoa majibu sahihi kwa wapiga kura wetu, mwenyekitindio ombi langu kwa mujibu wa kanuni nilizozitumia,”alisema.
Akijibu miongozo hiyo, Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge, alisema miongozo ya Mbatia na Shangazi imeangukia katika kanuni ya 47 (1) ambayo inasomwa pamoja na kanuni ya 48. “Lakini kanuni ya 47(4) inampa Spika mamlaka aridhike kama ombi hilo anaona jambo hilo kweli linahitaji kusitisha shughuli zilizo mbele yetu ili kujadili hoja hizo za dharura,”alisema.
Hata hivyo, alisema kwa hali anayoiona haoni kama suala hilo linahitaji kujadiliwa sasa. “Ni kweli tukio hili limegusa maeneo mengi, nawapa pole walioguswa kwa namna moja hata nyingine. Naamini Serikali iliyoko humu ndani itaitolea maelezo wakiangalia nchi nzima,”alisema na kuongeza kuwa, anaamini Serikali italizungumzia vizuri kuliko kila mbunge kujisemea katika eneo lake.
Kuhusu mwongozo wa Ngonyani, Chenge alisema kwa mujibu wa Kanuni ya 68 (7) ni lazima liwe tukio ama jambo ambalo limetokea mapema bungeni na si nje. Polisi asombwa, afa Wakati wabunge wakitaka kujadiliwa kwa athari za mvua zinazoendelea kunyesha, askari wa Jeshi la Polisi, Abbas Anas Haji (55) amekufa maji baada ya kusombwa akiwa na pikipiki yake aina ya Vespa wakati akipita eneo la barabara ya Fuoni Kibondemzungu lililofunikwa na maji. Tukio hilo limetokea jana majira ya saa 5:30 asubuhi wakati askari huyo akitokea kazini kwenda nyumbani kwake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Hassan Nassir Ali alisema marehemu alikuwa ni mfanyakazi wa jeshi la polisi katika Kitengo cha Picha, Makao Makuu ya Polisi upande wa Zanzibar.
Familia 150 zatangatanga Katika tukio jingine, zaidi ya familia 150 kisiwani Pemba zimekosa makazi na kulazimika kusitiriwa na ndugu na jamaa baada ya nyumba zao kuathirika vibaya na mvua kubwa iliyonyesha kwa siku tatu mfululizo.
Timu ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar iliyotembelea mikoa miwili Pemba na kujionea athari za mafuriko, imeelezea kufurahishwa na mshikamano mkubwa uliooneshwa na wananchi katika kusaidiana bila ya kujali itikadi za kisiasa.
Waziri asiye na Wizara Maalumu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Ali Juma Khatib alisema wananchi wameonesha uzalendo wa hali ya juu ambao watu wote walioathirika na mafuriko hayo wamehifadhiwa na kuishi kwa ndugu na jamaa.
Aidha, Khatib waliwataka wananchi walioathirika na mafuriko hayo wasirudi tena katika maeneo yao hayo ambayo athari zake bado zipo. Ameahidi kusaidia na kutoa mifuko ya saruji 50 kwa familia za wilaya ya Mkoani ili zikarabati nyumba zao.
Tanga-Arusha yafunguka Aidha, mkoani Tanga ambako miundombinu ya barabara ilisababisha kukusekana kwa usafiri kati ya mkoa wa Tanga na mikoa jirani ya Kilimanjaro na Arusha, hali imetajwa kurejea katika hali yake ya kawaida.
Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Robert Gabriel akizungumza jana katika mahojiano kwa njia ya simu alisema kiasi cha mvua inayonyesha kimeanza kupungua ingawa ipo hali ya mawingu mazito katika baadhi ya maeneo.
Naye Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba akizungumzia hali ya usalama kuhusu kifusi kilichoanguka na kufunga sehemu ya eneo la barabara kuu inayounganisha miji ya Soni na Lushoto alisema anaelekea eneo la tukio na kwamba atatoa taarifa.
Aidha, kuhusu mawasiliano ya barabara ya Tanga - Pangani alisema kwa sasa watumiaji wa barabara hiyo wanapita katika njia mbili mbadala ikiwemo ya Pongwe - Kirare jijini Tanga pamoja na ile ya Muheza- Misozwe - Pangani ya wilayani Muheza wakati huu ambapo Tanroads wanafanya jitihada za kutengeneza njia ya mchepuko katika eneo la daraja la Neema lililopo kwenye barabara kuu ya Tanga- Pangani.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Thobias Mwilapwa ameuagiza uongozi wa Jiji la Tanga kuacha kufanya kazi kwa mazoea badala yake wajitahidi kufanya utafiti wa maeneo ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja nyakati za msimu wa mvua badala ya kiangazi ili kupata picha ya mahitaji halisi ya ujenzi tofauti na inavyofanyika sasa.
Ametoa maagizo hayo kwa nyakati tofauti jana alipozungumza katika mahojiano na HabariLeo baada ya kutembelea baadhi ya mitaa ya jijini Tanga iliyoathiriwa na mafuriko yaliyotokana na mvua isiyo ya kawaida iliyonyesha mfululizo juzi kwa saa 24 na kusababisha maafa ikiwemo vifo vya wakazi wawili.
Katika mji wa Tanga, mvua hizo ziliua watu wawili, nyumba 97 zilizingirwa maji pamoja na Soko maarufu la vyakula la Magandini na kusababisha mali zote kupotea, nyingine 36 zilibomoka kabisa, moja kutitia, nyingine kuteketea kwa ajali ya moto uliotokana na hitilafu ya umeme ambapo kaya 59 zenye wakazi zaidi ya 200 walioathirika walihifadhiwa katika kambi zilizopo kwenye shule ya msingi ya Chumbageni, Kwakaheza, Magaoni, Mafuriko na Sekondari ya Hotten.
Mvua za kihistoria Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) hivi karibuni ilitoa taarifa inayoonesha kuwa, mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali mkoani Tanga zimefikia kiwango cha juu ambacho hakikuwahi kurekodiwa tangu mwaka 1949, sawa na takribani miaka 68 iliyopita.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Utafiti wa mamlaka hiyo, Dk Ladislauds Chang’a, mvua iliyonyesha kwa saa 24 Mei 9 mwaka huu mkoani Tanga ni ya milimita 316, kiwango ambacho hakijarekodiwa kwa miaka mingi.
Aliongeza kuwa, hawajafanya tathimini, lakini mwaka 2014 kulikuwa na kiwango kikubwa zaidi baada ya kunyesha mvua ya milimita 138 ndani ya saa 24 na kwamba kiwango cha juu kwa historia ya kituo cha Dar es Salaam ni mwaka 1953 iliponyesha mvua ya kiwango cha milimita 167.4. Alisema mvua za sasa zinatarajiwa kuendelea hadi mwishoni mwa mwezi huu.
Ijumaa, Mei 12, 2017
Watumishi wawili wa Serikali Mwambungu & Sozigwa waaga dunia
Mwambungu, Sozigwa wafariki dunia
IMEANDIKWA NA WAANDISHI WETUIMECHAPISHWA: 13 MAI 2017
TAIFA limepata pigo la kuondokewa na watumishi wa Serikali wa muda mrefu, mwanahabari nguli aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Kwanza wa Rais wa Awamu ya Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere, Paul Sozigwa na aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Saidi Mwambungu.
Wawili hao walifikwa na mauti katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) walikokuwa wamelazwa kwa matibabu. Sozigwa ambaye pia alikuwa Mkurugenzi wa Kwanza wa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD, sasa TBC baada ya kuwa Shirika la Utangazaji Tanzania), alifikwa na mauti jana saa nane usiku wa kuamkia jana kutokana na matatizo ya moyo , wakati Mwambungu pia aliaga dunia jana asubuhi kutokana na maradhi ya figo.
Msemaji wa JKCI, Anna Nkinda alithibitisha kutokea kwa vifo vya Mzee (84) aliyekuwa amelazwa tangu Aprili 25, mwaka huu akitokea Wodi ya Mwaisela ya Hospitali ya taifa Muhimbili (MNH) na Mwambungu (62) ambaye alifikishwa hospitalini hapo Mei 10 mwaka huu saa nane mchana.
Mtoto wa kwanza wa marehemu, Hamidu Mwambungu alisema baba yake alikuwa akisumbuliwa na tatizo la figo kwa zaidi ya mwaka mmoja na ni ugonjwa ambao umemsababishia mauti hayo.
Alisema familia inaendelea kupanga taratibu za maziko. “Hatujajua mazishi yatafanyika lini na wapi bado wanafamilia tunakutana kupanga lakini nadhani tunaweza kuzika mwishoni mwa wiki hii,” alisema Hamidu. Hamidu alisema msiba huo uko nyumbani kwa marehemu Tabata Kimanga, Dar es Salaam.
Mzee Sozigwa “Mzee Sozigwa alikuwa akisumbuliwa magonjwa mengine pia, aliletwa hapa akiwa na tatizo la moyo, akatibiwa hapa akawa amepona lakini alibaki hapa wakati akiendelea na matibabu ya yale magonjwa mengine mpaka leo (jana) alipofariki,” alisema Nkinda.
Mtoto wa marehemu, Mchungaji wa Kanisa la KKKT, Moses Sozigwa alisema baba yake alikuwa akisumbuliwa na magonjwa mbalimbali ikiwa ni pamoja na ugonjwa wa moyo, matatizo ya tumbo, na pia shida mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupoteza kumbukumbu inayotokana na kuwa na umri mkubwa.
Aidha, alisema familia inaendelea kupanga mazishi ya baba yao na kwamba msiba huo uko nyumbani kwake Mtoni Mtongani, Temeke kwenye Kanisa la KKKT ambako ni maarufu kama maskani ya Kwaya ya Lulu.
Mbali ya kuwa Mkurugenzi wa RTD na baadaye mwaka 1967 kuwa Mwandishi wa Habari wa Rais, Sozigwa alikuwa kada mzuri wa chama tawala, CCM alikokuwa Mwenyekiti wa chama hicho mkoani Pwani, lakini pia akiwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho. Sozigwa atakumbukwa kutokana na weledi na uadilifu wake katika kutimiza majukumu yake.
CCM kimetoa salamu za rambirambi kwa msiba huo wa Sozigwa ambapo Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole amesema kuwa chama kimepokea kwa masikitiko taarifa za msiba huo. “Mzee Sonzigwa alihudumia na kutoa huduma kwa utumishi uliotukuka ndani ya chama na pia serikali kabla na baada ya uhuru na pia alihudumia kama katibu wa kwanza wa Rais Mwalimu Nyerere,” alisema Polepole.
Alisema chama hicho kitamkumbuka na kumuenzi na jambo ambalo alishughulika nalo ni pamoja na kushughulikia misingi na maadili na miiko ya uongozi ndani ya CCM. Naye Naibu Katibu Mkuu CCM (Bara),Rodrick Mpogolo, amemtaja Mwambungu kuwa alikuwa kiongozi mwadilifu katika utendaji wake wa kazi ndani ya CCM alipokuwa Mkuu wa Utawala Makao Makuu (Ofisi Ndogo) Lumumba, Dar es Salaam na hata alipoteuliwa kuwa mtumishi wa Serikali.
“Tumempoteza kiongozi mahiri na shupavu … watu wanakumbukwa kwa yale mazuri unayofanya hapa duniani na Mwambungu atakumbukwa kwa mema aliyoyetenda wakati wa uhai wake,” alisema Mpogolo akiwa mjini hapa.
Naye Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) mkoa wa Morogoro, Christine Ishengoma, alisema alimfahamu Mwambungu wakati yeye (Dk Ishengoma) alipoteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani mwaka 2006 na aliyekuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete.
“Nimeshistushwa na kifo chake …ninaweza kusema kuwa Mwambungu ndiye aliyenipokea wakati nikiwa mkuu wa mkoa wa Pwani na yeye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha na makao makuu ya mkoa ni Kibaha,” alisema Dk Ishengoma.
Pamoja na hayo alisema kuwa, mara baada ya Mwambungu kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa na kupangiwa mkoa wa Ruvuma, Dk Ishengoma alisema alimpokea na kukabidhi mkoa huo wakati yeye akihamishiwa mkoa wa Iringa.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen Kebwe, alimtaja Mwambungu kuwa licha ya kumfahamu kupitia vyombo vya habari, alifahamiana yake wakati walipoteuliwa kuwa wakuu wa mikoa.
“Mwambungu alikuwa mcheshi, alikuwa karibu na wananchi na pia ni mpenda utani ni hazina kuu imepotea, lakini ni mapenzi ya Mungu,” alisema. Baadhi ya viongozi wa CCM, wakiongozwa na Mwenyekiti wao mkoa wa Morogoro, Innocent Kalogeries na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro mjini kichama, Fikiri Juma kwa nyakati tofauti waliwajulisha wajumbe walioshiriki kikao hicho juu ya kutokea kwa msiba huo.
Momogoro blog ;watendaji wa shule ya Lucky Vincent wapandishwa kizimbani
WAKATI Mkurugenzi wa Shule ya Msingi ya Mchepuo wa Kiingereza ya Lucky Vincent ya jijini Arusha, Innocent Mushi na Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo, Longino Nkana wakipandishwa kizimbani kutokana na vifo vya watu 35 wakiwemo wanafunzi 32 wa shule hiyo, ndege maalumu inatarajiwa kutua nchini leo kuwabeba majeruhi watatu wakatibiwe Marekani.
Mwinjilisti maarufu duniani kutoka Shirika la Samaritan Purse, Bill Graham wa Marekani na ndiye aliyebeba gharama za kukodisha ndege maalumu aina ya DC 8 kupeleka wanafunzi waliojeruhiwa katika ajali hiyo iliyotokea mwishoni mwa wiki iliyopita wilayani Karatu, Arusha.
Watoto hao wameumia shingo, miguu na sehemu mbalimbali za miili yao. Kwa mujibu wa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, Lazaro Nyarandu aliyezungumza jana na waandishi wa habari mjini Arusha, gharama za kukodisha ndege kwenda Marekani si chini ya dola za Kimarekani 350,000 (Sh milioni 700). Gharama hizo ni nje ya matibabu, chakula na malazi kwa wakati wote ambao wagonjwa hao na wasindikizaji watakuwa nchini humo.
“Tumefanikiwa kupata ndege aina ya DC 8 kutoka Shirika la Samaritan Purse linaloongozwa na mtoto wa Billy Graham aitwaye Franklin kwa ajili ya kuwasafirisha watoto Doreen Mshana, Sadia Awadh na Wilson Tarimo na wazazi wao watatu, yaani mama zao,” alisema Nyalandu akiwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Alisema pia watoto hao wataambatana na daktari wa hospitali ya mkoa wa Arusha ya Mount Meru, Elias Mashalla na muuguzi Simphorosa Silalye. Kwa mujibu wa Nyalandu, ndege hiyo inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro KIA) leo jioni ikitokea Charlotte ,Jimbo la North Carolina, Marekani.
“Endapo taratibu za safari ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa visa utafanikiwa, basi ndege inaondoka na wagfonjwa na wasindikizaji Jumapili (kesho) na baada ya kufika mjini Charlotte, North Carolina watasafiri kwa ndege nyingine maalumu ya kubeba wagonjwa hadi mji wa Sioux City, Iowa ambako watapokelewa na uongozi wa Hospitali ya Mercu na Shirika la STEMM,” alisema Nyalandu.
Alitumia fursa hiyo kuwataka Watanzania kupongeza juhudi za Rais, Dk John Magufuli, Makamu wake, Samia Suluhu Hassan na uongozi wa Mkoa wa Arusha chini ya Mkuu wa Mkoa, Mrisho Gambo kwa kuguswa na kushiriki katika kila hatua kuanzia baada ya ajali, mazishi hadi ufuatiliaji wa afya za majeruhi.
‘’Hili jambo ni letu sote hapa, hatuhitaji sifa bali tunachopaswa Watanzania wote kushirikiana kwa pamoja na kuweka mbele ubinadamu na kujitoa kwa hali na mali kuwasaidia hawa watoto ili waweze kupata nafuu na kurudi shuleni,” alisema Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Gambo alisema kuwa katika michango yote iliyochangwa kwa ajili ya rambirambi kwa msiba huo mpaka jana zilipatikana fedha kiasi cha Sh milioni 215.
Gambo alisema katika fedha hizo, kila familia ilikabidhiwa zaidi ya Sh milioni 3.8 na pia Serikali ilibeba gharama za usafiri, majeneza, mafuta ya magari na malipo ya madereva. Alisema Sh milioni 190 zilitumika katika matumizi mbalimbali ya msiba huo na kuwataka walioahidi kuchangia kutimiza ahadi zao.
Kizimbani Wakati majeruhi ambao ni wanafunzi wa shule hiyo wakitarajiwa kupelekwa Marekani, mmiliki wa shule hiyo na mwalimu mkuu msaidizi walipandishwa kizimbani kwa makosa kadhaa ya usalama barabarani, ikiwa ni pamoja na kusafirisha watoto bila ya kuwa na vibali.
Wakisomewa mashitaka yao jana mbele ya Hakimu Mkazi wa Hakimu Mkazi Arusha, Desdery Kamugisha, Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Rose Sule alidai watuhumiwa hao wawili wamefunguliwa kesi Namba 78/2017 huku Mkurugenzi wa shule hiyo akishitakiwa kwa makosa manne na Mwalimu Nkana akishitakiwa kwa kosa moja.
Akimsomea Mkurugenzi wa Lucky Vincent makosa yake, wakili huyo alidai kosa la kwanza ni la kuendesha gari la abiria bila ya kuwa na leseni ya usafirishaji ambapo Mei 6 mwaka huu katika eneo la Kwamrombo, Arusha Mjini akiwa mmiliki wa gari namba T 871 BYS aina ya Toyota Rosa, alifanya shughuli ya usafirishaji bila ya kuwa na leseni ya abiria.
Kosa la pili ni kuruhusu kuendesha gari bila ya kuwa na bima (Road Licence), Mei 6 mwaka huu akiwa mmiliki wa gari hilo aliruhusu gari hilo kuendeshwa bila ya kuwa na bima. Kosa la tatu ni kushindwa kuingia mkataba na mwajiriwa wake, Dismas Gasper ambapo Mei 6, 2017 akiwa mmiliki wa gari alishindwa kuingia mkataba na dereva huyo aliyeendesha gari lililopata ajali ambaye naye alifariki dunia katika tukio hilo.
Kosa la nne ni kubeba abiria zaidi ya 13 ambapo Mei 6 mwaka huu, mkurugenzi huyo ambaye ni Ofisa Msafirishaji na mmiliki wa shule ya Lucky Vincent alibeba na kusafirisha abiria zaidi ya 13 katika gari hilo kitendo ambacho ni kinyume na sheria.
Kosa la tano ni la Mwalimu Mkuu Msaidizi ambapo anashitakiwa kwa kuandaa safari iliyozidi abiria 13 ambapo ni kinyume cha sheria inadaiwa kuwa Mei 6 mwaka huu, Nkana akiwa Mwalimu Mkuu Msaidizi na mwandaaji wa safari alipakia abiria zaidi ya 13 kwenye gari lililosababisha vifo vya wanafunzi hao.
Baada ya washitakiwa hao kusomewa mashitaka yao yanayowakabili wakili anayewatetea washitakiwa hao, Method Komomogolo aliomba dhamana kwa washitakiwa hao huku Wakili wa Serikali Sule akisema hana pingamizi na dhamana yao.
Hakimu Kamugisha alitoa masharti ya dhamana kwa washitakiwa hao ambayo ni kila mshitakiwa alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wawili watakaosaini bondi ya Sh milioni 15 na kwamba hawatakiwi kuondoka nchini au ndani ya mkoa bila ruhusa ya mahakama pamoja na kuwasilisha hati zao za kusafiria.
Watuhumiwa hao walitimiza masharti ya dhamana yao na kesi yao kuahirishwa hadi Juni 8, mwaka huu.
Namna ya kuamsha hisia za mwanamke
Wanaume wengi huelewa kuwa kuna umuhimu wa kumuandaa mwanamke kwa kumshika shika maungo yake ya mwili lakini wengi hupuuzia suala hili kwa kuwa wao hamasa yao ya mapenzi huamka na mwili husisimka tayari kwa kuanza kushiriki tendo la ndoa mara tu baada ya kuona mwili wa mwanamke ukiwa mtupu.
Mwanaume wa namna hii huwa hawezi kumfikisha mwanamke kwani mara baada ya kumuingilia mwanamke ambaye hayupo tayari kuingiliwa kimwili kwa kuwa hajaandaliwa, mwanaume hujikuta anafikia mshindo ndani ya sekunde kadhaa na hata akitaka kuzuia bao hushindwa kufanya hivyo, hivyo hujikuta amemaliza haja zake za kimwili na kumuacha mwanamke pengine akiwa hata wazimu haujampanda na kwa bahati mbaya aking’amua hushindwa kurudia tena tendo kwani haitasimama tena.
Wataalamu mbali mbali wa mapenzi wanabainisha ya kuwa wanaume wenye kutumia muda mwingi kumuandaa mwanamke huweza kujizuia kufika mshindo mapema na hivyo hudumu kifuani kwa muda mrefu na hata kufanikiwa mfikisha mwanamke kileleni zaidi ya mara moja.
Hata hivyo muda wa kushikana shikana hutofautiana baina ya mwanamke na mwanamke, wanawake wengi husisimka kutokana na kushikwa matiti, matiti ya mwanamke mara nyingi ni yenye kusisimka sana endapo yatatomaswa vizuri kimahaba ama kwa kutumia mikono au mdomo kupekecha chuchu mithili ya mtu anayemung’unya pipi na wazimu ukianza mpanda ncha za matiti husisimka na kujitokeza yaani hudinda na hali hiyo hujitokeza sehemu zake za siri pia kwa mashavu ya k kupanuka na kuwa na hali ya kusisimka huku kinena kikimsimama na tezi zake hutoa ute.
Ute hutoka mahususi kuruhusu uume kupenya kwa urahisi, hata hivyo si wanawake wote huamsha hamasa ya mapenzi kwa kuchezewa matiti hivyo basi mwanamke anatakiwa kumwongoza mwanaume kwa maneno ama kwa kuweka mikono eneo anataka ashikwe ili apate hamasa ya mapenzi.
Aidha, wanawake wengine huwa hawana ujasiri wa kumwongoza mwanaume kumtomasa sehemu inayomnyegesha, hivyo kujinyima raha ya mapenzi. Hivyo mwanaume anapaswa kumshika shika mwanamke sehemu mbali mbali kama shingoni, mabegani na kumbusu sehemu ya juu ya mwili wake taratibu akiteremsha mikono kwenye sehemu za siri za mwanamke lakini ahakikishe hana kucha zenye ncha na vidole vikavu ili kutomuumiza mpenziwe na kusababisha ashki impotee gafla na asitake tena mambo!
Hapa ili zoezi liwe lenye mafanikio mwanamke anatakiwa kuonyesha ushirikiano kwa kutoa miguno ya kumchanganya mwanaume huku akitanua vema miguu ili mwanaume aweze kushughulika vema na sehemu inayozunguka kinena, hadi atakapobaini mabadiliko ya moyo wa mke, ngozi kuwa na joto, pumzi kuongezeka, uso kukunjamana mithili ya mtu anayeumia na anaweza lia kwa utamu anaousikia na hapo mwanaume anaweza kumwingilia kwani huwa tayari kuingiliwa kimwili.
Askari polisi asombwa na maji unguja_zanzibar
UNGUJA: Polisi mmoja kwa jina Abbasi Anali amefariki dunia kutokana na kusombwa na maji huko Unguja, Zanzibar.
Taarifa zilizotufikia zinaonesha kwamba askari huyo ambaye alikuwa mpiga picha wa Polisi, alikuwa akiendesha pikipiki maarufu kama Vespa, kutoka mjini Unguja kuelekea Makunduchi.
Mwandishi wa habari Bi Jazaa aliyefika katika eneo la tukio hilo anasema, “Ajali hiyo imetokea leo hii Ijumaa tarehe 12 Mei, 2017…na ilikuwa baina ya saa 5 na 6 hivi.” Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Hassan Nassir, amethibitisha kifo cha askari huyo, na kuongeza kwamba tayari mwili wake umepatikana.
Uchunguzi wa mwili huo unaendelea katika Hospitali ya Mnazi Mmoja. “Mauti yamemfika alipojaribu kuvuka katika eneo la Kibonde mzungu, Fuoni ambapo kulikuwa na maji mengi,” Jazaa.
Watu walioshuhudia tukio hilo wanasema eneo hilo lliikuwa limetapakaa maji kutokana na mvua kunyesha na kuziba barabara kuu. wanasema asakari huyo amekosa mwelekeo wakati anavuka na kutumbukia kwenye maji mengi.
Mvua kubwa inayoendelea kunyesha hasa kwenye maeneo ya ukanda wa Pwani, imesababisha madhara mengi ikiwa ni pamoja na vifo katika baadhi ya maeneo, nyumba kuanguka, magari kukwama au kuharibika, na miundombinu mingi kuharibika, hususan barabara.
Mamlaka ya Hali ya Kewa Tanzania imetoa taarifa inayoonesha ukanda wa Pwani unaendelea kupata mvua za kiasi cha 50mm ndani ya kipindi cha saa 24. Na kwakesho tarehe 13 May, 2017, “kuna Angalizo la Matarajio ya kuwepo Vipindi vifupi vya Mvua kubwa,” Kwa mujibu wa taarifa za tovuti yao.
Kwa upande wa Zanzibar, maeneo yaliyoharibika zaidi ni pamoja na Mwanakwerekwe, Kibonde mzungu, Ziwa maboga, Mtoni kidato, Jeng’ombe, na Sebleni kwa wazee.
Nitumie maoni yako kwa kubonyeza Jina ilo apo chini
NazirHamza
Jambazi wakike auawa jijini Nairobi
Katika Facebook, mwanamke huyo anajitambulisha kama mwanafunzi wa zamani wa chuo kikuu

Mwanamke anayedaiwa kuwa jambazi sugu, ambaye amekuwa akipakia mtandaoni picha zake akiwa amejipodoa na kujipamba, ameuawa na polisi jijini Nairobi nchini Kenya.
Kijana huyo ambaye ametambuliwa kama Claire Mwaniki aliuawa na polisi alfajiri na mapema Jumatano katika mtaa wa kayole.
Gazeti la kibinafsi la Daily Nation linasema mwanamke huyo alikuwa na majambazi wengine wanne wa kiume pale walipofumaniwa na polisi wakitekeleza wizi katika eneo la Lower Chokaa, mtaa wa Kayole.
Anadaiwa kufyatulia risasi maafisa wa polisi akiwa na jambazi mwingine lakini wawili hao wakauawa.
Wenzao walifanikiwa kutoroka.
Taarifa katika gazeti la Daily Nation inasema polisi waliwaandama baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wenzao kupitia WhatsApp kwamba majambazi hao walikuwa wamekwepa mtego waliokuwa wamewekewa.
Polisi walijiandaa na kisha wakawakabili katika mtaa wa Lower Chokaa.
Mkuu wa polisi wa mtaa wa Kayole Joseph Gichangi amenukuliwa na gazeti la Daily Nation akisema: "Kwa mujibu wa wadokezi wetu, mwanamke huyo alikuwa mke wa mshukiwa wa ujambazi ambaye anafahamika vyema, ambaye bado anasakwa na polisi."
Alisema visa vya wanawake kujihusisha na magenge yanayotekeleza wizi wa kutumia mabavu vinaongezeka.
Wakenya mtandaoni wamekuwa wakisambaza picha za Mwaniki na kumjadili sana mtandaoni.
Katika Facebook, mwanamke huyo anajitambulisha kama mwanafunzi wa zamani wa chuo kikuu cha Nairobi na mtu anayependa kufurahia maisha.
Kuna wakati alipakia picha yake, ya mwanamume na mtoto, na kuongeza kwamba hiyo ni "familia".
Mkuu wa polisi Nairobi Japheth Koome anasema magenge mengi ya wahalifu huwa na wanawake.
"Wanawake hutumiwa kusafirisha silaha, kukusanya habari na hata kushiriki katika ujambazi," Bw Koome alisema.
Aliongeza kuwa wakati mwingine hutumiwa na majambazi wa kiume kuwapelekea chakula mafichoni.
Nitumie maoni yako Kupitia
Facebook kwa kubonyeza Jina ilo apo chini Nazir-Hamza
Betri za simu aina ya smartphone zinazochaji simu ndani ya dk 5
StoreDot walitoa mfano wa siku ikiwekwa chaji kwa kutumia chaja maalum
Betri za simu za kisasa za Smartphone ambazo zinaweza kujaa chaji katika muda wa dakika tano pekee huenda zikaanza kuuzwa sokoni mwaka ujao.
Teknolojia hiyo iliwekwa kwenye maonesho mara ya kwanza mwaka 2015 na kampuni ya Israel ya StoreDot.
Kampuni hiyo iliwasilisha kwenye maonesho ya kila mwaka ya teknolojia mpya ya CES mjini Las Vegas betri hiyo maalum iliyopewa jina FlashBattery.
Afisa mkuu mtendaji wa kampuni hiyo Doron Myersdorf ameambia BBC kwamba sasa wanatarajia kuanza kuzalisha na kuuza betri hizo mapema mwaka 2018.
Hata hivyo, Ben Wood, mchanganuzi wa teknolojia katika kampuni ya CCS Insight amesema ana shaka kidogo kuhusu ahadi hiyo.
Bw Myersdorf amesema hawezi kufichua kwa sasa ni kampuni gani ambazo zimepata idhini ya kutengeneza betri kwa kutumia teknolojia hiyo.
Mwaka 2015, aliambia BBC kwamba betri hizo za kampuni yake zimeundwa kwa kutumia viungo ambavyo vinawezesha kufanyika kwa shughuli za kemia kwa haraka isiyo ya kawaida na pia kuhamishwa kwa nguvu za umeme kutoka sehemu moja hadi nyinginwe kwa kasi sana.
Baadhi ya miundo ya betri hizo ilikuwa kubwa kuliko betri nyingi za smartphone za wakati huo, lakini Bw Myersdorf anadai sasa wameandaa betri ambazo zinaweza kuanza kuuzwa sokoni.
"Tutachaji simu ya smartphone kwa dakika tano," alisema.
Aliongeza kwamba teknolojia hiyo tayari inafanyiwa majaribio na watengenezaji betri wawili China na kwamba utengenezaji kwa wingi wa betri hizo unatarajiwa kuanza robo ya kwanza ya 2018.
Lakini ingawa Bw Wood ana shaka kwamba betri hizo zinaweza kuuzwa haraka hivyo, amekiri kwamba iwapo betri hizo zitafanya kazi kama ilivyoahidiwa, basi utakuwa ni ufanisi mkubwa sana katika sekta hiyo.
"Kubahatisha kuhusu teknolojia ya betri kunaweza kukudhuru. Nimejifunza kuwa na shaka kila wakati kuhusu ahadi hizi. Hebu tusubiri," aliambia BBC.
Alieleza kuwa muundo wowote ambao unatoa joto kwa wingi unaweza kuathiri utendakazi wa betri.
Dot pia wanadai wameunda betri ya gari inayoweza kujaa chaji kwa dakika tano pekee
Kuna kampuni nyingine zinazojizatiti kuunda betri ambazo zinajaa chaji kwa haraka.
Novemba, Qualcomm walitangaza betri za Quick Charge 4 ambazo zinaahidi betri hiyo itajaa chaji kwa dakika tano na kusalia na chaji kwa saa tano.
StoreDot pia walizindua betri ya gari ambayo inajaa chaji kwa dakika tano katika maonesho ya teknolojia mjini
TANESCO YATOA OMBI KWA WANANCHI WOTE
SHIRIKA la Umeme Tanzania, (TANESCO), limewaomba wateja wake na wananchi kwa ujumla kutoa taarifa mapema mara inapotokea hitilafu ya umeme iliyosababishwa na mvua au sababu nyingine.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo Mei 11, 2017, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka, (pichani juu), alisema, sambamba na hilo pia wananchi wasifanye shughuli au kukaa chini ya miundombinu ya umeme.
“Lakini tunawaomba wananchi watoe taarifa haraka maeneo yenye mafuriko au mkusasnyiko wa maji mengi ili wataalamu wetu waweze kuchukua hatua za haraka.” Alisema.
Dkt. Mwinuka pia alisema endapo kuna nyaya, nguzo au kifaa chochote cha umeme kimepata hitilafu na kinahatarisha maisha ni vema uangalizi au alama ikawekwa ili kuwapa hadhari wapiti njia na watoto wasikaribie eneo hilo wakati mafundi wa TANESCO wakichukua hatua za marekebisho.
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Tanzania (TMA), katika taarifa yake iliyotoa Mei 9, 2017 imeonya kuwa maeneo ya Pwani ya Kaskazini ikiwemo visiwa vya Unguja na Pemba, yatakabiliwa na vipindi vifupi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24 kuanzia Mei 10 hadi 12, 2017.
Aidha kwa upande wake, mtaalamu wa masualaya umeme kutoka TANESCO, Mhandisi Simon Kihiyo, amewahakikishia wananchi kuwa miundombinu ya TANESCO iko imara na salama, na hitilafu zinazotokea za hapa na pale nyingizinasababishwa na sababu za kibinadamu, au za kimazingira kama vile nguzo za umeme kugongwa na magari, au miti kuangukia nguzo.
"Naomba nitoe angalizo kwa wateja wetu, kama pametokea hitilafu yoyote ya umeem nyumbani kwako, ni vema ukatoa taarifa TANESCO au ukamtafuta fundi wa umeme mwenye taaluma badala ya kushughulikia tatizo hilo wewe mwenyewe ilihali ukiwa huna utaalamu na masuala ya umeme, kwani hiyo ni hatari."
Naye kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO Leila Muhaji amesema, katika kipindi hiki cha mvua kuna athari ndogo ndogo zimetokea kwenye miundombinu ya TANESCO hususan nguzo za umeme, lakini akatoa hakikisho kuwa mafundi wa TANESCO wanekuwa wakichukua hatua za haraka kurekebisha athari katika miundombinu ya umeme pindi tu zinapotokea.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Dkt. Tito Mwinuka, (katikati), akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Me11, 2017. Dkt. Mwinuka ametoa hadhari kwa wananchi kutogusan miundombinu ya Tanesco hususan nyaya zilizoanguka, au kufanya shughuli yoyote karibu na miundombinu yab umeme katika kipindi hiki cha mvua kubwa zinazoendela kunyesha nchini. Kulia ni Mhandisi Simon Kihiyo, na kushoto ni Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila Muhaji.
Mhandisi Simon Kihiyo, akitoa ufafanuzi wa kitaalamu kuhusu hatua za kuchukua pindi hitilafu ya umeme inapotokea
Dkt. Mwinuka (kushoto) na Mhandisi Kihiyo, wakati wa mkutano huo leo
Dkt. Mwinuka akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake
Waandishi wa habari wakiwa kazini
Waandishi wa habari wakiwa kazini
Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila Muhaji, akitoaufafanuzi zaidi wa hatua za kuchukua endapo wateja au wananchi wataona hitlafu ya umeme kwenye maeneo yanayowazunguka
Mhandisi Kihiyo, (kulia0na Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO Leila Muhaji katika mkutano na wanahabari
Mhandisi Simon Kihiyo, (kulia), Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila Muhaji (kushoto) na Afisa Uhusiano wa Shirika hilo, Henry Kilasila wakijadiliana jambo.
Alhamisi, Mei 11, 2017
Polisi yadaka mwanafunzi akifanya njama ya kuuza bastora
Bastola
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linamshikilia mwanafunzi wa Chuo cha St Joseph, Lewis Mbise (23) akituhumiwa kukutwa na bastola moja aina ya Luger cz 100 yenye namba C 4122 ikiwa na risasi 13 ndani ya magazine, mali ya baba yake kwa lengo la kuiuza.
Pia linawashikilia walimu wawili na mwanafunzi kwa tuhuma za kuvujisha mtihani wa Kidato cha Sita unaoendelea. Akizungumzia tukio la mwanafunzi kukamatwa na bastola, Kamanda wa kanda hiyo, Kamishna Simon Sirro aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba mwanafunzi huyo alisema alikamatwa Mei 5 maeneo ya Mbezi Magari Saba katika Manispaa ya Ubungo baada ya kupata taarifa kuwa kuna kijana anauza silaha.
Kamanda Sirro alisema baada ya taarifa hizo, jeshi hilo lilifuatilia na kumpata kijana huyo na katika mahojiano, alikiri kuwa bastola hiyo aliiba nyumbani kwa baba yake mzazi pamoja na fedha kiasi cha Sh 800,000. “Ni watu wengi wanatumia silaha, lakini hawatunzi silaha ni kitu ambacho kinatakiwa kutunzwa.
Tayari nimeagiza baba wa kijana huyu akamatwe kwa hatua zaidi, niwasihi na wengine wanaotumia silaha kuhakikisha silaha hizo zinahifadhiwa vizuri,” alieleza Kamanda Sirro. Alisema upelelezi unaendelea kufanyika ili kubaini lengo la mtuhumiwa kuiba silaha hiyo ikiwamo kujua kama kuna taarifa ya kupotea kwa silaha hiyo kabla haijapatikana.
Sirro alisema watuhumiwa waliokamatwa kwa tuhuma za kuvujisha mitihani ni walimu Musa Elius (35) na Innocent Mrutu (33) mkazi wa Kibamba na mwanafunzi Ritha Mosha.
Kamanda Sirro alisema watuhumiwa hao walinaswa Mei 6, maeneo ya Chang’ombe baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Ofisa wa Baraza la Mitihani la Taifa, Aron Mweteni kuwa Mei 5, katika Shule ya Sekondari Chang’ombe alimkuta Elius akiingia darasani na mwanafunzi Mosha ambaye ni mtahiniwa wa mtihani wa Kidato cha Sita unaoendelea, wakiwa na karatasi yenye maswali na majibu ya somo la Kemia kwa Vitendo.
Alisema baada ya kuwakamata na kuwatilia shaka, ufuatiliaji wa awali ulifanyika kupitia Baraza la Mitihani la Taifa na kubainika kuwa swali hilo ni miongoni mwa maswali ya mitihani ya Kidato cha Sita unaofanyika mwaka huu.
Mitihani hiyo ilianza Mei 2, mwaka huu na itakamilika Mei 19, mwaka huu. Kamanda Sirro alisema watuhumiwa wote wanaendelea na mahojiano na upelelezi utakapokamilika watachukulia hatua za kisheria.
Marubani kutoka Tanzania wapata ujuzi namna ya kuendesha ndege
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Balozi Dkt. Agustine Mahiga akizungumza wakati wa mkutano baina ya wawakilishi kutoka Tanzania na Afrika Kusini kuhusu majadiliano ya awali ya mikataba na makubaliano ya ushirikiano baina ya Tanzania na Afrika Kusini yanayotarajiwa kutiwa saini kesho wakati wa Ziara ya Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini anayetarajiwa kuwasili leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Afrika Kusini Maite Nkoana – Mashabane
SERIKALI ya Jamhuri ya Afrika Kusini imekubali kuendelea kuwafudisha marubani wa Tanzania ikiwa ni sehemu moja wapo ya kukuza maendeleo ya sekta ya uchukuzi na usafiri wa anga pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Augustine Mahiga ameyabainisha hayo leo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa ufafanuzi kuhusu majadiliano ya awali yaliyofanyika kati ya nchi hizo mbili juu ya mikataba mbalimbali inayotegemewa kusainiwa Mei 11 mwaka huu.
Balozi Mahiga alisema kuwa katika majadiliano hayo wamejadili mikataba iliyowahi kusainiwa kwa kupima utekelezaji wake pamoja na kujadili mikataba mipya iliyojikita katika sekta mbalimbali za maendeleo zikiwemo za uchukuzi, nishati, elimu pamoja na mawasiliano.
“Katika sekta ya uchukuzi tumekubaliana kuboresha barabara, usafiri wa anga pamoja na reli hasa ya TAZARA, sisi tumenunua ndege na tunaendelea kununua zingine zitakazosafiri hadi Afrika ya Kusini hivyo nchi hiyo imekubali kuendelea kuwafundisha marubani wa Tanzania kuendesha na kukarabati ndege hizo,”alisema Balozi Mahiga.
Nitumie maoni yako Kupitia
Fb.com













